Kima cha chini cha mshahara chaongezwa Ufaransa

0
1376

Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa ametangaza kushusha kodi na kuongeza kiwango cha kima cha chini cha mshahara kwa wafanyakazi kwa kiasi cha Euro 100 kwa mwezi.

Akitangaza hatua hiyo katika hotuba yake ya kwanza tangu maandamano  yaanze nchini humo Macron amesema malipo kwa watumishi wanaofanya kazi kupita saa za kazi yataongezwa pamoja na kuboresha maslahi ya wastaafu.

Waziri Mkuu wa Ufaransa Eduado Phillipo ametangaza kusitishwa kwa maandamano hayo na kuweka ulinzi katika maeneo yote ya Paris.