Kansela Angela Merkel afanya ziara nchini Ugiriki

0
1099

Kansela Angela Merkel  wa Ujerumani amefanya ziara nchini  Ugiriki  kuonyesha mshikamano na nchi hiyo baada ya kipindi kigumu cha kubana matumizi na kuipa msaada wa kidiplomsia kuhusu ubadilishaji wa jina wa taifa jirani la Macedonia.

Merkel pia amefanya  mazungumzo na waziri Mkuu Alexis Tsipras kujadili hatua inayosubiriwa ya kubadili jina la taifa hilo la Macedonia iliyokuwa sehemu ya Jamhuri ya zamani ya Yugoslavia .

Merkel alizuru mji mkuu wa Macedonia, Skopje kabla ya kura ya maoni juu ya kubadili jina kuonyesha uungaji wake mkono ambapo bado  suala hilo linasababisha mgawanyiko nchini Ugiriki ambako mojawapo ya vyama vinavyounda muungano wa Tsipras kinapinga na kutishia wingi wake wa bungeni.

Wakati huo huo polisi  nchini Ugiriki imewatawanya  kwa kutumia mabomu ya machozi mamia ya waandamanaji waliokuwa wakipinga ziara hiyo ya Merkel