Idadi ya vifo yazidi kuongezeka nchini Morocco

0
512

Kufuatia tetemeko la ardhi nchini Morocco, idadi ya watu wanaokadiriwa kufariki dunia katika tetemeko hilo inakadiriwa kufika watu 2,900.

Wale walionusurika wamejiunga na timu ya uokozi ili kuendeleza juhudi za kuwatafuta manusura wengine. Vikosi vya uokoaji vimeendelea kufanya kazi ya uokozi bila kuchoka, hata usiku kucha.

Ni muhimu kukumbuka kwamba hili ni tukio baya zaidi kuwahi kuikumba nchi ya Morocco, Kaskazini mwa Afrika, tangu tetemeko la ardhi la mwaka 1960 lililoharibu mji wa Agadir na kusababisha vifo vya maelfu ya watu.