Dola Mil 10 za USAID kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi

0
386

Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) limetangaza uwekezaji mpya katika miradi miwili wenye thamani ya Dola Milioni 10 za Kimarekani, ili kulinda ikolojia muhimu na kupunguza gesi ukaa nchini.

Uwekezaji huo umetangazwa na Naibu Kiongozi Mkuu wa USAID, Isobel Coleman.

Fedha hizo zinajumuisha kiwango cha awali cha Dola Milioni 8 za Kimarekani za uzinduzi wa mradi wa USAID Tumaini kupitia vitendo, ambao ni wa miaka mitano unaoendeshwa kwa ubia na Taasisi ya Jane, na Dola Milioni 2.1 za Kimarekani kwa ajili ya kuboresha uwezo wa jamii za Pwani na wavuvi wa Tanzania katika kuhimili na kukabili mabadiliko ya tabianchi kama sehemu ya mradi unaoendelea wa USAID Heshimu Bahari.