Kituo cha mabasi cha Nanenane Dodoma kufanyiwa marekebisho

0
860


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma dokta Binilith mahenge amemtaka Mkuu wa Wilaya wa Dodoma mjini, Patrobas katambi na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin kunambi kukifanyia maboresho kituo cha mabasi yaendayo mikoani cha Nanenane Jijini Dodoma.

Dokta Mahenge amesema hayo Jijini Dodoma katika ziara yake ya kukagua vituo mbalimbali vya mabasi yaendayo mikoani ambapo ameshuhudia kwa dosari kadhaa katika kituo hicho.

Dokta Binilith Mahenge ilimlazimu kuamka mapema alfajiri na kufika katika kituo kikuu cha mabasi ya abiria waendao mikoani na nchi jirani cha Nanenane ili kushuhudia huduma ya usafirishaji wa abiria na usalama wao.

Amehimiza amehimiza kufanyika ukarabati ambao utaondoa dosori ndogo ndogo alizozishuhudia katika vituo hivyo na kuaagiza wamiliki wa mabasi kuanza kutoa huduma kwa njia ya kieletroniki ili kurahisisha huduma na kuiongezea serikali mapato.