Ulipo mwili wa Kashoggi bado kitendawili

0
2180

Zikiwa zimepita siku kadhaa tangu kuuawa kwa mwandishi wa habari wa Saudi Arabia katika mazingira ya kutatanisha ndani ya ubalozi mdogo wa nchi hiyo mjini Istanbul,- Uturuki, bado mwili wake haujulikani ulipo.

Licha ya serikali ya Saudi Arabia kukiri kuwa mwandishi huyo wa habari aliuawa ndani ya ubalozi huo na kisha mwili wake kukatwa vipande vipande, imeshindwa kuthibitisha mahali mwili wake ulipo.

Saudi Arabia imesema kuwa ipo tayari kuilipa fidia familia ya Kashoggi pamoja na mchumba wake aliyekuwa akitarajia kumuoa hivi karibuni, fidia kutokana na kifo hicho.