Waziri Bashungwa atembelea kambi za mabondia

0
230

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa, Naibu Waziri wa wizara hiyo Abdallah Ulega pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Yusuph Singo leo Desemba 24, 2020 wametembelea kambi za mazoezi za mabondia Abdallah Shabani Pazi(Dulla Mbabe) iliyoko Mwananyamala na Mfaume Mfaume iliyoko Manzese jijini Dar es salaam na kuwatakia heri katika mapambano yao ya kimataifa yatakayofanyika Desemba 26, 2020 Next Door Arena, Dar es salaam.