Jaji Mkuu Mstaafu, AUGUSTINO RAMADHANI amesema ni jambo la kawaida hasa katika nchi za jumuiya ya madola kuunda jopo maalum kuchunguza majaji wanaotuhumiwa kwenda kinyume na taratibu za kinidhamu.
Jaji RAMADHAN alikuwa akitoa ufafanuzi kuhusu uamuzi wa serikali ya KENYA kumsimamisha kazi na kisha kumchunguza Naibu Jaji Mkuu wa serikali ya nchi hiyo NANCY BARAZA ambaye anatuhumiwa kumtishia kwa bastola mmoja wa walinzi jijini NAIROBI, mwishoni mwa mwaka jana.
Jaji RAMADHANI ni mmoja wa wajumbe saba wa jopo lililoteuliwa na serikali ya KENYA kuchunguza tuhuma zinazomkabili BARAZA.
