
Mkuu wa mkoa wa mwanza injinia Evarist Ndikilo amewaapisha wakuu wapya wa wilaya za mkoa huo na kuwataka watekeleze majukumu yao huku wakizingatia hofu ya Mungu.
Injinia Ndikilo amewaelekeza wakuu hao saba wa wilaya kuwa katika kutekeleza majukumu yao, utatuzi wa kero za wananchi na kujituma zaidi ndiyo kitakuwa kipimo cha ufanisi wao.
Majina ya wakuu hao wapya wa wilaya za mkoa wa mwanza ambao wamekula kiapo cha utii na utumishi wa umma tayari kuanza kazi ya kuwatumikia wananchi na wilaya zao katika mabano ni Amina Masenza (Ilemela), Karen Yunus (Sengerema), Seleman Mzee Seleman (Kwimba), Mary Tesha (Ukerewe), Jacqline Liana (Magu), Baraka Konisaga (Nyamagana) na Mariam Lugaila (Misungwi).
Estom Sanga, TBC Mwanza
Local General
Naibu waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI Aggrey Mwanri amewaagiza madiwani nchini kuwa wakali katika kusimamia matumizi ya pesa za halmasha...
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DR. Ali Mohamed Shein amesema licha yakuweko mfumko m...
Mkuu wa mkoa wa Dodoma Dr Rehema Nchimbi amewaapisha Wakuu saba wa wilaya mkoani kwake ikiwemo wilaya mpya ya Chemba na kuwataka wajitahidi kuonekana kwa wananch...
Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi Goodluck Medeye amepiga marufuku raia yeyote kutoka nje ya nchi kupewa ardhi ya kuwekeza bila ya idhini ya mkuu wa mk...