
Mkutano wa 34 wa Makanisa ya Kiprotestanti nchini Ujerumani, Kirchentag, umefunguliwa rasmi mjini Hamburg nchini humo, huku ukiwa umebeba agenda kadhaa ikiwemo kudorora kwa amani na tishio la ongezeko la matabaka kati ya matajiri na masikini duniani.
Mkutano huo wa siku tano, unaozishirikisha zaidi ya nchi 85 duniani kote wakiwemo wajumbe kutoka Tanzania, umelenga kujadili njia bora za kuhakikisha kuwa dunia inakuwa mahali bora na salama pa kuishi
Mitaa ya Jiji la Hamburg Ujerumani, kuzunguka viunga vya Ziwa Alster, zaidi ya watu laki tatu kutoka mataifa mbalimbali duniani, wamemiminika kuhudhuria mkutano mkubwa ulioandaliwa na Makanisa ya Kiprotestant huko Ujerumani.
Baadhi ya wajumbe waliohudhuria mkutano huo, wamebainisha namna bora ya kuhakikisha kuwa uhasama wa kidini, na baadhi ya viongozi wa serikali kutojali matatizo yanayowakabili wananchi wao vinakomeshwa.
Awali wakiongea na vyombo vya habari kutoka nchi mbalimbali katika ukumbi wa Congres Center Hamburg, Rais wa Makanisa ya Kiprotestanti Ujerumani Profesa Dokta Gerhard Robbers na Katibu Mkuu wake Dokta Ellen Ueberschar, wameelezea nia yao ya kuendeleza mijadala inayogusa maisha ya watu kiroho na kimwili.
Ben Mwaipaja, TBC Hamburg Ujerumani.
Kenya
Idadi ya watu waliokufa nchini China kwa tetemeko la ardhi lililotokea katika Jiimbo la Sichuan imeongezeka kufikia watu 207 majeruhi wakiwa zaidi ya elfu kumi na moja...
Kikosi cha upelelezi nchini Marekani- FBI kinasubiri kufanya mahojiano ya kina na mtuhumiwa wa milipuko iliyotokea mjini humo siku ya jumatatu wakati wa mashindan...
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry amewasili Korea Kusini wakati huu ambapo mgogoro baina ya Korea Kaskazini na Korea Kusini unaripotiwa kuendelea.
Ker...
Rais wa mpito nchini Venezuela, Nicolas Maduro na mpinzani wake Henrique Capriles wametoa hotuba zao za mwisho kwa wapiga kura wao kabla ya kufanyika kwa uchaguzi kesh...
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)