Tanzania Broadcasting Corporation - (TBC)

Thursday
Sep 09th
Text size
  • Increase font size
  • Default font size
  • Decrease font size
Home You and Your Family Kucheza soka la kulipwa si lelemama

Kucheza soka la kulipwa si lelemama

Kiungo wa timu TAIFA ya TANZANIA , NIZAR KHALFAN

Kiungo wa timu TAIFA ya TANZANIA anaecheza soka la kulipwa nchini CANADA, NIZAR KHALFAN amesema kucheza soka la kulipwa kwenye nchi ya kigenini sio lelemama hata kidogo.

NIZAR amesema yeye amekutana na mambo mengi ya kukatisha tamaa ila alipigana hadi kufanikiwa na kusema wachezaji wa TANZANIA wajitume zaidi na kucheza nafasi nyingi uwanjani.

Kiungo huyo anaecheza soka kwenye klabu ya VOUNCOVER WHITE CAMPS amesema nafasi ipo kwa wachezaji wa TANZANIA kucheza soka nchini CANADA ila kinachotakiwa ni umakini wao na kujituma zaidi uwanjani na nje ya uwanja.

Pia kiungo huyo amesema yeye hatomsahau kocha anaeondoka wa TAIFA STARS, MARCIO MAXIMO ambae anasema amechangia kwa kiasi kikubwa mafanikio yake. NIZAR alikuja hapa nchini kwaajili ya mchezo wa kirafiki wa KIMATAIFA dhidi ya BRAZIL ambao amesema umetoa changamogo tosha kwa wachezaji wa TANZANIA.

 
Banner