
Kocha MANUEL PELLEGRIN ametimuliwa kazi katika timu ya REAL
Rais wa REAL MADRID –FLORENTINO PEREZ ametangaza kutimuliwa kibarua kwa PELEGRIN na kuanza rasmi kwa mchakato wa kuwa na MOURINHO siku 5 baada ya kuonekana akiondoka na MOURINHO katika gari lake baada ya fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya baada ya MOURINHO kuonekana akitokwa na machozi wakati akiwaaga wachezaji wake.
Timu ya INTER MILLAN inataka ilipwe EURO millioni 16
Lakini pamoja na yote hayo MOURINHO ndio kocha mpya wa REAL MADRID ambapo bodi ya wakurugenzi wa klabu hiyo imemtangaza kuwa anakuwa kocha wao huku wakiwa tayari kwa fungu lolote kuwa naye huku mazungumzo yakiendelea na atatambulishwa rasmi muda wowote kuwa ni kocha wa REAL.



