Tanzania Broadcasting Corporation - (TBC)

Monday
Sep 06th
Text size
  • Increase font size
  • Default font size
  • Decrease font size
Home You and Your Family Liverpool wahofia kumkosa Torres

Liverpool wahofia kumkosa Torres

Mchezaji wa Liverpool,Fernando Torres

LIVERPOOL ina wasiwasi ya kusubiri uchunguzi wa goti la mshambuliaji wa timu hiyo FERNANDO TORRES ambaye amefanyiwa uchunguzi  huo na daktari bingwa siku ya Jumatatu.

Tatizo hilo la TORRES lilimfanya aondolewe katika orodha ya wachezaji waliocheza na FULHAM ambapo timu hizo zilitoka sare ya bila kufungana.

Lakini pamoja na kupata matibabu nchini HISPANIA, nyota huyo hivi sasa atafanyiwa tena uchunguzi baadaye wiki hii huku daktari bingwa wakiwa na matumaini ya kugundua tatizo.

Taarifa ya klabu hiyo imesema kuwa TORRES alifanyiwa uchunguzi na daktari bingwa wa goti jana mchana nchini HISPANIA na anapata matibabu lakini jeraha lake litachunguzwa tena wiki hii.

Mchezo mwingine wwa LIVERPOOL utakua siku ya Jumatatu ambapo itakua nyumbani kucheza na WESTHAM UNITED, lakini mchezo wa muhimu kwa timu hiyo ni ule wa nusu fainali ya ligi ya EUROPA dhidi ya ATLETICO MADRID timu ya zamani ya TORRES utakaochezwa April 22.

Last Updated ( Tuesday, 13 April 2010 11:40 )  
Banner