
Waziri Mkuu wa zamani nchini GUINEA CELLOU DALEIN DIALLO pamoja na mwanasiasa mkongwe wa chama cha upinzani nchini humo ALPHA CONDE wanatarajiwa kuchuana katika marudio ya uchaguzi mkuu nchini humo.
Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa jana usiku na Tume ya Uchaguzi nchini humo wanasiasa hao wanaongoza miongoni mwa wagombea ISHIRINI NA WANNE waliojitokeza kuwania nafasi ya urais ambapo DIALLO amepata Asilimia 39.72 wakati CONDE ana Asilimia 20.67 ya kura.
Uchaguzi wa awali ulifanyika tarehe ISHIRINI NA SABA mwezi uliopita ambapo matokeo ya uchaguzi huo yametangazwa baada ya kuongezewa siku mbili na Mahakama ya Rufaa ili kuiwezesha Tume ya Uchaguzi kuhesabu kura.
Uchaguzi huo ni wa kwanza wa kidemokrasia kufanyika nchini



