Tanzania Broadcasting Corporation - (TBC)

Monday
Sep 06th
Text size
  • Increase font size
  • Default font size
  • Decrease font size
Home Kenya Chama cha Rajapakse chaongoza-Srilanka

Chama cha Rajapakse chaongoza-Srilanka

Rais wa Srilanka,Mahinda Rajapakse

Matokeo ya awali ya uchaguzi uliofanyika jana nchini SRI-LANKA, yanaonyesha kuwa chama cha Rais MAHINDA RAJAPAKSA, wa nchi hiyo, kinaongoza kwa kura katika uchaguzi wa wabunge.

Chama hicho kimepata asilimia 60, ya kura zilizokwisha hesabiwa hadi sasa.

Chama cha aliyekuwa mpinzani mkuu wa Rais huyo wa SRI-LANKA, katika uchaguzi wa Rais uliofanyika hivi karibuni , Jenerali SARATH FONSEKA kimepata asilimia tano ya kura zilizokwishahesabiwa.

Hata hivyo waangalizi wa uchaguzi wamesema uchaguzi huo haukuwa huru wala wa haki. Wamesema zaidi ya nusu ya watu wa jamii ya TAMIL, ambao wamelazimika kukimbia makwao kutokana na  vita,  hawakupata fursa ya kushiriki katika uchaguzi huo.

Last Updated ( Wednesday, 14 April 2010 08:44 )  
Banner