Tanzania Broadcasting Corporation - (TBC)

Monday
Sep 06th
Text size
  • Increase font size
  • Default font size
  • Decrease font size
Home Africa Politics EAC yakabiliwa na changamoto ya kudumisha ushirikiano

EAC yakabiliwa na changamoto ya kudumisha ushirikiano

Balozi wa KENYA hapa nchini MUTINDA MUTISSO Balozi wa KENYA hapa nchini MUTINDA MUTISSO amesema nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki zinakabiliwa na changamoto ya kuendeleza ushirikiano baina yake hususan wakati huu wa kuishindani katika nyanja mbalimbali za kiuchumi ili kumudu ushindani kimataifa.

 

 

Balozi MUTISSO ametoa kauli hiyo katika mahojiano na TBC kuhusu ushirikiano uliopo kwa nchi zinazounda jumuiya hiyo ambazo tayari zimeanza kutekeleza itifaki ya soko la pamoja.

Akizungumzia uelewa mdogo miongoni mwa wakazi wa AFRIKA MASHARIKI juu ya maana ya soko huria, Balozi MUTISSO amesema serikali na asasi zilizopo zinawajibika kusambaza elimu kuhusu mchakato wa shirikisho na jinsi ushirikiano huo unavyofanya kazi.

 

 

 

 

 

 

 

 


Last Updated ( Thursday, 08 July 2010 17:24 )  
Banner